TB JOSHUA IMAGES WI MSG

WATCH EMMANUEL TV LIVE-TB JOSHUA

SIKU NILIYOKUWEPO KWA TB JOSHUA APRIL 2012

Wednesday, June 19, 2013

PICHA ZA IBADA YA JUMAPILI KANISA LA YESU KRISTO LA HUDUMA YA MAOMBEZI NA UPONYAJI KWA NABII FLORA PETER

Jumapili hii ilikuwa ni ya kipekee. Mungun aliweza kutembea kwa kila mmoja. Wingu lilitanda katika kanisa hili. watu walionekana kububujika kutoka na uwepo wa Mungu ulikuwepo mahali hapa. Ninaomba tushirikiane kwa kupitiam picha hizi
Nabii Flora (kushoto) na Msaidizi Mchungaji Jury

Jina la kanisa: Kanisa la Yesu Kristo la Huduma ya Maombezi na Uponyaji
Eneo: Mbezi Salasala
Kituo: Shuka kituo cha Mbezi Mbuyuni barabara ya kuelekea Tegeta
Jina maarufu: Ukifika uliza Kanisa la nabii Flora
Simu: Nabii Flora Peter: +255 65744699 Octavian: +255716 310661
Blogu: www.nabiiflora.blogspot.com
Facebook: Nabii Flora Peter
Youtube: www.youtube.com/Nabii Flora Peter

Mpiga Picha wetu: Rumafrica Simu yake
Simu:+255 715851523
Blogu www.rumaafrica.blogspot.com au www.rumaafricajobs.blogspot.com




Dada huyu alikuwa na tatizo la moyo kutanuka na miguu, alipofika kwa nabii Flora aliombewa na sasa anasema hajisikii tena maumivu ya moyo bali miguu. Mungu anazidi kumponya.

Dada huyu ni mkazi wa Dodoma aliyekuja kwa Nabii Flora akiwa na tatizo la kuvimba mguu. Mguu huu ulikuwa na uvimbe mkubwa zaidi ya hapo. Nabii Flora alimuombea na sasa uvimbe unapungua. Mungu ni mwema.

Mama aliyefunga safari kutoka Songea mpaka Dar es Salaam kwa nabii Flora kwa kutka Nabii Flora amuombee mwanae aliyekuwa kiwete na hawezi kutembea kutoka na miguu kujikunja. Baada ya maombezi miguu ilijikunjua na sasa anasimama

Mwigizaji wa Luniga akishuhudia matendo makuu ya Mungu baada ya kuombewa na nabii Flora. anasema biashara zake zinaenda vizuri kabisa. Hapo mwanzo alikuja kwa nabii Flora akiwa amechoka kifedha.

Mama huyu akionyesha alama ya tick iliyotokea katika mkono wake baada ya Nabii Flora kutamka na kutabiri kuwa kuna watu watawekewa alama ya tick katika mikono yao kama ishara ya kukubaliwa na Mungu katika mahitaji yao.





Nabii Flora akiwa amempakata mtoto aliyekuwa akiumwa ugonjwa wa kuanguka kifafa na usiku kuzimia. Kulia ni mama wa huyu mtoto aliyemleta kwa Nabii Flora na kuombewa na sasa ni mzima hana kifafa na hazimii usiku.

Watu wakiwa wameangushwa kwa Nguvu za Mungu wakati Nabii Flora akiomba na kukemea mapepo

Nabii Flora akiwaombea watu wenye mangonjwa mbalimbali ambapo aliwaomba washike sehemu ya kutolea damu.



Nabii Flora akiombea watu na kukemea mapepo

Kipindi cha kuombea wale waliofika madhabahuni kumtolea Mungu mafungu ya kumi.

Watu wakiwa wamedondoshwa na nguvu za Mungu baada ya Nabii Flora kuhesabu mara tatu

Nabii Flora akiwa kaika maombezi

Nguvu ya Mungu ikifanya kazi kwa kupitia mtumishi wake Nabii Flora Peter.

Watu wakiwa wametoka katika viti vyao na kusimama koridoni kwaajili ya kupokea baraka za Mungu kwa kupitia mtumishi wake nabii Flora Peter.



Nabii Flora Peter akiwa amesimama juu ya kiti akimwaombea watu, na hii ni kutokana na watu kutomuona hasa waliokaa nyuma.




Kwaya Kuu ya hapa kanisani.







Apostle Gideon Mutalemwa akiongoza sifa

Mtumishi wa Mungu cameraman Octavian

Tuesday, June 18, 2013

BISHOP ZACKARY KAKOBE NDANI JIJI LA TORONTO CANADA KWA KAZI YA MUNGU


Mkutano mkubwa kufanyika Toronto Canada chini ya Bishop Zackary Kakobe.Siku ya jana akizungumza na vyombo vya habari kueleza jinsi anavyo jisikia furaha kufika na jinsi alivyo jipanga kuhubiri kwa siku mbili June20 7:00Pm at Tennis Canada Grounds,Sunday June23 7:00Pm at Toronto on M3N 3A6.Tizama Video ya Press Conference baada ya kufika Toronto Canada. Picha za mapokezi ya Bishop Zackary Kakobe baada ya kufika Toronto Canada.











Bishop Zackary Kakobe akizungumza na vyombo vya habari.


Big Up Jimmy

2013 MANA CONFERENCE


EDSON MWASABWITE AMSHUKURU MUNGU KUONGEA NA STARA THOMAS KWAAJILI YA KAZI YA MUNGU



Namshukuru kwa nafasi na wakati mwingine alionijalia hata sasa. Leo nimeongea na Stara Thomas kuhusu kushirikiana nae katika nyimbo yangu mpya, namshukuru kwa kukubali hilo na tutakwenda kurekodi wimbo pamoja naye ili kuzidi kumsifu Mungu na kumwimbia pamoja. Kaa tayari kwa hilo pia event tutakayoifanya pamoja nae mwezi ujao jijini mbeya ya kusifu na kuabudu. Mungu wangu wa mbinguni akubariki sana mpendwa.

Stara Thomas

SAMSASALI KUFUNJA UKIMIA SIKU YA JUMAPILI

Hello marafiki na wasomaji wote wa Blog hii!!

Leo ninawaletea habari njema zilizoambatana na mwaliko maalum kwa watu wote wenye mapenzi mema na Samuel Sasali, The Blogger, MC,Mzee wa Ideas mengi ambaye mara zote husema Mungu alimnyima urefu akamjalia Mdomo (kuongea sana) na kukosa aibu pia!!!

Baada ya sarakasi za kutosha za kutafuta mwenzi wa kumfaa hatimae pacha wangu amegota na kumpata mlimbwende wa pekee aliyewashinda wanawake zaidi ya Bilioni 4 duniani na kuwa wa pekee...Usukani mdogo unaoendesha Merikebu kubwa!!!
Ndio ni binti huyu Dk Milembe John Madaha ambaye ameteka moyo wa kaka Mkubwa na kwa huyu Papaa amegeuka rapper,mwana mashairi na mtiifu sana!!Kama una kumbukumbu nzuri, blog hii imewahi kum-ZOOM kijana huyu kama mmoja ya vijana wanaopaswa kuigwa na vijana wengine,fuata link umfahamu vema;
.http://chavalamedia.blogspot.com/2012/08/salaam-leo-katika-kipengele-hiki.html
Basi habari njema ndio hii, jumapili hii wewe na wenzako wote ambao ni marafiki wa kweli Samuel Sasali au ni msomaji wake wa Papaa On Tuesday au ni Mwanachama wa Marafiki Huru au ni mpenzi wa Friends On Friday au umewahi kufundishwa na yeye popote pale,shuleni, chuoni au kanisani au hata kama amewahi kusherehesha shughuli yako yeyote ile..basi sasa ni saa ya kumuunga mkono kwa kumaanisha!!

Ni jumapili hii ya tar 23/06/2013 kuanzia saa nne asubuhi pale Mbezi Beach A katika kanisa la VICTORY CHRISTIAN CENTRE TABERNACLE (VCCT),Unaweza ukapanda gari mpaka mwenge na kupanda usafiri wa kanisa unaondoka hapo tatu na nusu ama ukachukua bajaji mpaka huko kanisa la hema,au ukapanda gari mpaka kawe mwisho na kupanda bajaji pia mpaka kanisani au ukashuka Mbezi Tanki bovu na kuchukua bajaji au bodaboda mpaka kanisani...lakini kama unakuja na private car njoo na barabara ya Mwai Kibaki(zamani old bagamoyo road) kisha baada tu ya daraja utaona kibao kushoto kwako kama ukitokea mwenge then fuata njia hiyo kwa hakika huwezi kupotea!!

Ni marufuku kuja mikono mitupu na ni marufuku kuja peke yako,namaanisha jaribu kubeba zawadi ya pongezi na usiache kuwajulisha wengine wanaomfahamu Papaa!!
Haitakuwa siku ya kawaida kwa hakika maana Papaa ni baadhi ya vijana nguli ambae tayari alikuwa kwenye kundi la ma-senior bachelors na sasa rasmi anaanza kuaga aga kundi hilo....na hata harusi yake itakuwa mwishoni wa October, kama hakutakuwa na badiliko lolote basi itakuwa 26TH OCTOBER.. hivyo mwenye macho na asome na kuelewa!!!

Mimi binafsi kwa niaba yangu mwenyewe na kwa niaba ya Blog hii na wafanyakazi wote wa Chavala Ideas Platform ninatamka baraka nyingi kwa rafiki yangu mkubwa na pacha wangu Samuel pamoja na Shemeji yangu,his wife to be ....Mungu awaonekanie katika kila hatua ya michakato hii mpaka hapo watakapooana!!!

Na kwa hakika tuko bega kwa bega,naam tuko tayari kutoa mchango wowote ule wa hali na mali utakaohitajika ili kufanikisha shughuli hii,KWA HAKIKA NINAMKUBALI SANA PAPAA KWA JINSI ALIVYO NA ALIVYO MCHAKARIKAJI,HE IS AMONG MY BEST FRIEND IN TOWN!!!Kwa wale msiomfahamu zaidi basi msiache kutembelea Blog yake kila siku"samsasali.blogspot.com"

NA MWALIKO HUU NIMEUTOA KWA HIARI YANGU KWA NIABA YAKE,HIVYO KAMA UKIKWAMA AU UKIWA NA SWALI LOLOTE NAMNA YA KUFIKA HAPO KANISANI BASI USISITE KUWASILIANA NASI,NASI TUTAKUSAIDIA KUFIKA!!

+255 713 883 797 King Chavala-MC

Source:...http://chavalamedia.blogspot.com/2013/06/hatimaye-samuel-sasali-aka-papaa.html

ALICHOKISEMA UPENDO BENSON KATIKA FACEBOOK

Ooh Yesu nakupendaaa, Ulinipenda kwaanzaaa
Napenda siku zooootee, nikutumikieeeeeee!

Najaribu kutafakari kuhusu maisha yangu najikuta nazidi kumpenda sana Mungu... coz kama ni maisha ya raha na ya shida nayajua vizuri sana.. kuishiwa mpaka senti ya mwisho najua.. kula mchicha tu najua, kulala njaa najua, kwenda kula nnachotaka pale Hyatt regency au Serena najua, kula maharagwe na ugali najua, kula pizza na burger najua, kupanda ndege najua, kutembea kwa miguu najua, kukaa kwenye kiyoyozi najua, kupigwa jua na vumbi najua, kupata hela najua, kuumizwa najua, kupendwa najua, kulipa kodi ya nyumba najua, kulipa umeme, maji, tv channels, internet...najua. LAKINI PAMOJA NA KUPITIA HAYO YOOOTE, MUNGU ALIKUWA UPANDE WANGU NA MKONO WAKE HAUKUPUNGUKA HATA SIKU MOJA, NA NDIO MAANA LEO NAMTUKUZA. ACHA DUNIA YOTE IJUE KWAMBA NAKUPENDA EE MUNGU WANGU ULIYENIUMBA.



RON KENOLY NA DON MOEN KUMPA TAFU ASKOFU KAKOBE NCHINI CANADA ALHAMIS HII


Mwimbaji nguli wa muziki wa injili duniani Ron Kenoly anatarajiwa kuwa mmoja wa waimbaji watakaoimba katika mkutano mkubwa wa injili wa kimataifa ulioandaliwa na askofu Zachary Kakobe ambao unatarajiwa kuanza alhamisi hii tarehe 20 hadi 23/6/2013 katika uwanja wa Rexall Centre Tennis katika jiji la Toronto nchini Canada.

Waimbaji ambao tayari wametajwa kuimba katika mkutano huo ambao umepewa jina la "Toronto Miracle Healing Crusade"ni pamoja na nguli mwingine Don Moen, kundi la wanandugu Krystaal, Martha Munniz na waimbaji wengineo, mkutano huo utakuwa wa kwanza kufanyika katika uwanja huo wa tennis huku pia askofu Kakobe kupitia huduma yake ya BZKIM inafanya kuwa muhubiri wa kwanza kutoka Tanzania na Afrika mashariki na kati kufanya mkutano mkubwa sehemu ya wazi kama ilivyo kwa watanzania kushuhudia wahubiri wakubwa wakija kuhubiri nchini.

Wiki iliyopita askofu Kakobe alikaririwa akiwatoa hofu waumini wake kutokana na madai ya kwamba amewatoroka na kuwaambia kwamba anakwenda kutimiza agizo la Mungu kuhubiri Canada katika mkutano mkubwa tena akitumia lugha ya Kiswahili. Kama hukusoma BONYEZA HAPA.

Monday, June 17, 2013

MEXICO SCHOOL OF MINISTRY DR. CERULLO MINISTERED A POWERFUL WORD


From the Mexico School of Ministry Dr. Cerullo ministered a powerful word "There’s an awesome power here in Mexico. God is going to do something for His people in Mexico He have never done before. God will open the windows of heaven on Mexico. God’s people are going to see themselves as they are and not as the devil deceives them to believe!"

Ndani ya chuo cha huduma huko Mexco (Mexico School of Ministry), malefu ya watu wamepokea mpenyo wa Kiroho. Wengi wameshuhudia kwamba mambo yanayondeka hayajawahi kutokea. Hakika Mungu ameamua kuwatembelea watu wake.

Kilichonifurahisha ni pale uwepo wa Mungu ulipoenea kwa kila mtu, kiasi kwamba kila mmoja aliweka mikono yake kwa mwingine, maana katika agano jipya, sote tuliomwamini Yesu Kristo ni Makuahani.

"Uongozi wa Blog hii tunamtakia Mtumishi Cerullo maisha marefu yenye uliznzi wa Mungu, ili aendelee kuihubiri kweli ya Neno la Mungu".

ABOUT DR. MORRIS CERULLO
Dr. Morris Cerullo is a man on the move for God. He is a man whose entire life is dedicated to fulfilling the call of God to take the Gospel of Jesus Christ to every living creature.

With over 60 years of ministry God has used Dr. Cerullo to pioneer overseas ministries & open many countries that have been considered closed to the Gospel.

Dr. Morris Cerullo, was raised in a Jewish Orthodox Orphanage until the age of 14 1/2 when he gave his life to Christ.
Because of his faith, he was punished and eventually left the orphange.
Since his call to the ministry at the age of 15, God has used Morris Cerullo to reach multitudes of people around the world in over half a century of ministry. To realize the impact of what this ministry has done is staggering.

Consider:
* Dr. Cerullo has ministered to innumerable multitudes of people face to face.
* Miracle Crusades in which the lame walk, the blind see, the deaf hear, and the Gospel is preached have reached up to 500,000 people in one service.
* Dr. Cerullo has ministered in scores of countries on six continents in person, via satellite, television, radio and literature.
* Over one million Nationals have been trained in his Schools of Ministry.
* Dr. Cerullo has personally ministered to Presidents, Prime Ministers, and heads of state in many nations.

Ministering alongside Dr. Morris Cerullo for over 57 years has been his wife, Theresa. Theresa Cerullo is an energetic and effective part of the Morris Cerullo World Evangelism ministry, serving as the official Corporate Secretary/Treasurer. She is lovingly referred to as "Mama" by the millions of Nationals around the world.
"Sir, you are a blessing to our generation.
May God's blessings increase abundantly in your life.
We love you".

"WEKEZENI MASHAMBANI" MASANJA MKANDAMIZAJI


Emmanuel Mgaya maarufu kama Masanja Mkandamizaji

Emmanuel Mgaya maarufu kama Masanja Mkandamizaji amesema kuwa vijana wanapaswa kufikiria namna ya kuwekeza mashambani kwenye fursa za kutosha kuliko kuendekeza majivuno yasiyo na msingi.

Akizungumza na Starehe Masanja alisema anafurahi kwani mwaka huu amefanikiwa kuvuna tani kadhaa za zao la mpunga katika shamba lake lililopo Mbarali Estate.

“Nimelimia Mbarali Estate namshkuru Mungu kwa kufanikiwa kuvuna mpunga wangu baada ya kuwekeza shamba lenye ukubwa wa ekari 15, huu ni uwekezaji mzuri unaotoa matunda kwa muda mfupi iwapo utahudumia shamba lako ipasavyo.”

“Vijana wengi wana nguvu na uwezo wa kuingia mashambani ila wanaendekeza ‘usharobaro’ kitu ambacho hakina mavuno kwao,” alisema Masanja aliyetumia mashine ya kisasa katika zoezi hilo.

Masanja ambaye pia ni mwimbaji wa kwaya ya New Jerusalem alisema: “Mimi ni mchungaji mtarajiwa lakini huduma yangu ya uchungaji nimeanzia kwenye kundi langu hili la Ze Komedy, kupitia hilo nina washirika wangu ambao natamani wawe kama mimi mchungaji wao wafuate nyayo zangu, naomba maombi ya watumishi wengine wamuombee Joti,” alisisitiza!

Kwa sasa, Masanja anahudhuria ibada katika kanisa la EAGT, Mito ya Baraka pia amefanikiwa kutoa nyimbo 10 za Injili na tayari album yake ya ‘Hakuna Jipya’ iko mitaani.

Inatoka: Gospel Vision TZ

PASTOR STEVEN WAMBURA, JAMES KALEKWA, FRED MSUNGU NA MC PILIPILI WAFANYIKA BARAKA KWENYE KINGDOM EXPLOITS.

Katika Chuo cha Mt. Agustino-Mwanza, kulikuwa na Event iliyopewa Jina la Kingdom Exploits, iliyoandaliwa maalum kabisa kwa ajili ya Vijana waliopo chuoni hapo. Tukio hili lilianza Mida ya Saa 2:00 Usiku hadi Saa 5:00 Usiku huku Wanenaji wakiwa ni Bw. James Kalekwa-Mwanza, Fred Msungu-Dar na Mch. Steven Wambura-Dar.

Mchekeshaji wa Kimataifa toka Tanzania, Dar es salaam Bw. Emmanuel Mathias a.k.a Mc Pilipili alikuwepo Ukumbini hapo kuvunja mbavu za Wanafunzi wa Chuo hicho. Shughuli ilifanyika katika Ukumbi wa M10, na Praise Team iliyoundwa na Vijana wa Tafes, Casfeta, Huima na Uscf iliuongoza Umati wa Vijana waliokuwepo katika kuusogelea Uso wa Mungu.

Sasa tazama picha hizi uone jinsi Mambo yalivyokuwa chini ya Mc wa Event Bw. Barnabas Shija.

Mc wa Event Bw. Barnabas Shija

Wanafunzi waliohudhuria

Presentation ya Bw. James Kalekwa

Huyu jamaa hata kwenye Uimbaji yuko vizuri. Ni Fred Msungu

Bw. Fred Msungu akihudumu

Wakati wa Panel Discussion

Mc Pilipili akiingia kwenye Jukwaa tayari kufanya mambo yake 

Mc Pilipili baada ya kumaliza Show yake

Bw. James Kalekwa akihudumu katika Uimbaji

Pastor Wambura akiwaombea Wanafunzi wa SAUT

Kutoka Kushoto ni Barnabas Shija, Pastor Wambura na Mc Pilipili

Team Tukio

Kuanzia Kushoto ni Pastor Steven Wambura, Mc Pilipili, James Kalekwa, Billy, Fred Msungu, Adolph Nzwalla na Sowane Emmanuel.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...
There was an error in this gadget