RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

USEJA WA MAPADRI SASA KATIKA MJADALA, WANAWAKE NAO RUKSA KUWA MAASKOFU

Wimbi la mabadiliko hayo limeyakumba makanisa hayo mawili baada ya viongozi wao wakuu kulazimika kufanya maamuzi mazito juu ya mapadri na maaskofu wanaoyatumikia , ambapo tayari wanawake wameruhusiwa kuwa wachungaji na maaskofu, huku suala la mapadri kutoruhusiwa kuoa likipata ruksa ya kujadiliwa.

Wimbi hili la mabadiliko limekuja wakati mmoja, ambapo kwa upande wake kanisa Anglikana tayari limeruhusu rasmi wanawake kuwa wachungaji na maaskofu , wakati kanisa katoliki nalo limeruhusu mjadala juu ya ama mapadri wake waendelee na utaratibu wa kutooa au waoe.
Vyombo vya habari vilielezea tukio hilo kama moja ya matukio makubwa katika karne ya 21 kwa kanisa Anglikana, lililoanza tangu miaka 20 iliyopita na hatimaye kukamilika hivi karibuni.
Shirika la habari la kimataifa la sky News limemkariri Askofu Welby akisema kuwa amefurahishwa sana na matokeo ya kura hizo na kwamba ni mwanzo mzuri wa shughuli kubwa ijayo.
Nayo Televisheni ya kimataifa ya CNN katika moja ya vipindi vyake vilivyoripotiwa juu ya tukio hili ilibainisha kwamba huenda kanisa Anglikana likawa na maaskofu wengi wanawake kuanzia mwishoni mwa mwaka huu.

Source: Strictly Gospel

Comments