RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MTOTO MWENYE KANSA YA MACHO AFARIKI DUNIA MUHIMBILI DAR ES SALAAMA

MTOTO Godwin Florence Rweyemamu (3), mkazi wa Kijiji cha Kamala, Kata ya Bangwe mkoani Kigoma aliyeletwa katika Hospitali ya Taifa jijini Dar es Salaam kwa matibabu ya kansa ya macho amefariki dunia leo asubuhi.

Mtoto Godwin amefariki baada ya kusumbuliwa na kansa ya macho iliyoambatana na malaria na upungufu wa damu mwilini.

Mtoto Godwin Florence Rweyemamu (3) enzi za uhai wake akiwa na bibi yake, Elda Charles Rweyemamu.

Godwin aliletwa na bibi yake Elda Charles Rweyemamu katika Hospitali ya Muhimbili hivi karibuni wakitokea mkoani Kigoma kwa ajili ya matibabu lakini uchunguzi wa madaktari uligundua kuwa wamemchelewesha hivyo arudishwe nyumbani Kigoma.

Katika harakati za bibi yake kutafuta nauli ya kurudi Kigoma, wananchi walimchangia shilingi milioni 1.2 ikiwa ni pamoja na tiketi ya ndege na walipaswa kuondoka na Ndege ya Shirika la ATC jana Jumamosi saa 11 alfajiri, kabla ya muda huo kufika, saa 9 usiku marehemu alizidiwa kutokana na kuishiwa damu pamoja na malaria ambapo alipelekwa Zahanati ya St. Monica, Manzese kisha Hospitali ya Mwananyama, hali ilipozidi kuwa mbaya alipelekwa Muhimbili.

Marehemu anatarajiwa kuzikwa kesho Jumatatu katika makaburi ya Mbezi-Makabi jijini Dar.
Bibi wa mtoto huyo ametoa shukrani kwa wale wote waliojaribu kuokoa maisha ya mjukuu wake kwa maombi na michango ya hali na mali.

Kwa yeyote anayependa kuwasiliana na bibi huyo atumie namba 0762 175 117, 0784 420 215 au 0719 285 100.

SOMA HISTORIA YA MTOTO HUYU NA UONE ALIVYOTESEKA ENZI ZA UHAI WAKE. BONYEZA HAPA KUJUA MENGI

Comments