Binafsi nimefurahi sana kuona Elizabeth Michael (Lulu) kuhudhuria katika matamasha ya Gospel. Lulu ni msanii mkubwa sana Tanzania katika ulimwengu wa filamu za Kibongo yaani Bongo Movie. Msanii huyu ambaye ametokea kujulikana tangia akiwa mdogo sana katika uigizaji ameweza kuwapata wapenzi wengi sana wanaopenda kazi zake. Kitu kingine kilichonifurahisha kutoka kwa Lulu ni pale tu alipoweza kucheza na kufurahi na Watanzania wenzake huku akionyesha kukuubali uimbaji wa Bony Mwaitege. Lulu alijikuta akivutiwa sana na mwimbaji wa nyimbo za Injili Ambwene Mwasongwe kwa uimbaji wake, hii ilimfanya amfurahie na aliweza kumfuata na kufanya naye mazungumzo naye kidogo na kupokea upako kutoka kwa Ambwene.
Siku ya Jumapili ilikuwa siku ya kipekee sana kwa mwimbaji wa nyimbo za Injili Bony Mwaitege alipokuwa akizundua DVD yake ndani ya ukumbi wa Diamond jijini Dar es Salaam. Tamasha hili liliweza kuwakusanya watu wengi sana wakiwemo Watumishi wa Mungu, wasanii wwa Bongo Movie, waimbaji wa nyimbo za Injili na watu mbalimbali. Tamasha hili likuwa na mvuto wa kipekee. Uimbaji wa Bony Mwaitege uliwagusa watu wengi sana na hasa mavazi yake yalitokea kupendwa sana.
Bony Mwaitege ni mwimbaji mkongwe Tanzania na ni mwimbaji mwenye kupendwa sana na watu wengi kwa uimbaji wake na kucheza kwake.
Lulu akifanya yake
Lulu akipokea upako kutoka kwa Ambene Mwasongwe wakati akiimba stejini
Kutoka kulia ni mwimbaji wa gospel Upendo Kilahiro, Lulu na Ambwene Mwasongwe
Lulu akiwa na Ambwene Mwasongwe
Lulu akiwa na Emmanuel Mbasha
Picha kwa hisani ya Uncle Jimmy
BONYEZA "Read More" HAPO CHINI KIDOGO-KUSHOTO KUONA MATUKIO MENGINE YA TAMASHA HILI LA BONYY MWAITEGE
Comments