RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

KANISA LA MLIMA WA MOTO ASSEMBLIES LAFANYA MAOMBEZI NA KUKEMEA NDOTO MBAYA

Jamani kuna watu wana kiu ya kumuona Mungu akifanya mambo makuu katika maisha yao. Hii ilionekana katika Ibada Takatifu iliyofanyika katika  kanisa la Mlima wa Moto Assemblies of God lilipo Mikocheni "B" Dar es Salaam Tanzani kwa Askofu Mh. Dkt. Gertrude Rwakatarea, watu waliweza kufanya wawezavyo kwa kutaka kumugusa Mungu wetu kwa njia ya maombi.
Katika ibada zozote tunaamini kwamba kila mtu anaingia ibadani akiwa na hitaji lake muhimu ambalo anataka Mungu wetu wa Mbinguni ametendee.
Hii ilijitokeza katika kanisa hili la Mungu baada ya askofu wa wakanisa hilo Mh. Dkt Gertrude Rwakatare alipomaliza kuwaombea, aliwaomba waumini wa kanisa hilo kuomba kile wanachotaka Mungu awafanyie. Kanisa lilijawa na kelele za maombi ambapo kila mtu aliweza kuomba kile anachotaka Mungu amsaidie.
Kama Wakristo tunaamini katika maombi kuna nguvu za ajabu sana, na kuna mambo mengi sana yanaweza kutookea baada ya kufanya maombi.
Kitu cha kuzingatia katika maombi ni kuiandaa imani yako iamini kuwa huyu ninayemuomba yupo hata kama kwa macho haonekani, ila kwa ulimwengu wa Rohoni anapatikana. 
Unatakiwa kujitakasa mbele za Mungu kabla hujaanza maombi yako binafsi ufanyiwe na Bwana, ikiwezekana tafuta mahali patulivu ili unaomba kusiwe na mwingiliano wa mawazo mengine wakati ukiomba, baada ya kumaliza kuomba jenga imani yako kuwa jambo lako Mungu kisha lifanya juu yako, usiwe mtu wa kulalamika unapoona hitaji lako halijafikia kwa wakati.
Kila mtu anatambua kuwa Mungu wetu hana upendelea, ni Mungu wa haki kwa kila mmoja, kwahiyo unapoomba na wenzako utambue ya kuwa Mungu atawapa wote. Tuombe sana Mungu maombi yetu yasiwe ya mashindano, bali wewe omba ukimwangalia Mungu tu.
Kuna mengi tuweza kuongea na wewe, lakini unaombwa sana kutembelea blogu yetu ya www.mountainoftanzania.blogspot.com
www.rumaafrica.blogspot. com

 




BONYEZA "Read More" HAPO CHINI KUONA MWENDELEZO WA MATUKIO HAYA














 





















Comments