RUMAFRICA Magazine

RUMAFRICA FASHION

RUMAFRICA FASHION

MAISHA SAFARI NDEFU

Jina langu la lililoko katika cheti cha kuzaliwa ni Rulea Sanga, niliyezaliwa Makete miaka mingi  iliyopita, na baada ya hapo mama yangu ambaye kwa sasa ni marehemu alikuja kuhamia katika kijiji cha Mtili "A" ambako mimi na mama yangu tukaweka makazi yetu hapo.

Namshukuru kaka yangu Marehem Amir Sanga, alinipeleka shule ya msingi na kuanza masomo yangu mwaka 1988 katika shule ya Msingi Mtilia "A". Nakumbuka siku ya kwanza napelekwa niliingizwa katika ofisi ya Mwalimu Mkuu Kondo na kuandikishwa. Nilionyeshwa darasa langu na baada ya siku chache nilichanguliwa kuwa Kiongozi wa darasa (Monitor) kwahiyo kazi yangu ilikuwa kusimamia kazi zote za wanafunzi wenzangu wa darasa na pia kuwapelekea madaftari yao kwa walimu ili yasahihishwe.

Katika uongozi wangu huo nilichukia sana kazi ya kuandika majina ya wapiga kelele kwani kulikuwa na lawama sana na kulikuwa na watu wenye nguvu ambao ukiandika majina yao tu, ujue siku yako mitaani itakuwa mbaya. Nakumbuka siku moja nilimwandika dada mmoja anaitwa Bety, dada alikuwa na ubavu sana, baada ya kumuandika aliadhibiwa na mwalimu. Bety siku moja nikiwa natoka darasani kueleka nyumbani alinishika shati na kunitwanga kichwa katika mdomo wangu, na mdomo wangu kupasuka pale pale, nililia sana…Nilipofika nyumbani nikiwa nimepasuliwa mdomo niliogopa kumwambia mama yangu kwani niliona aibu kusikia nimepigwa na mwanamke, nilimdanganya mama yangu, lakini baadae alikuja kujua chanzo cha kupasuliwa kwa mdomo wangu. Mama alinihudumia na baadae nilipona. Na mpaka sasa nina kovu lake.

Nilipofika darasa la tatu nilikuwa ni mtu mwenye wivu sana katika masomo. Sikuwa mtu mzuri sana kimasomo lakini nilitamani kuwa mtu wa kwanza katika masomo. Darasani kwetu kulikuwa na watu waliokuwa akili sana, na baadhi yao ni Chesco Sanga (mtoto wa pili wa kaka yangu wa kwanza katika familia yangu), Christina Komba, Rehema Komba, Kaja Mtavangu, Shida Mahenge (huyu ni dada ambaye alikuwa tishio darasani), hawa ndio walioonekana kunisumbua sana. Lakini mimi nilikuwa nashinda sana na mtoto wa kaka yangu, Chesco Sanga, sikutamani aonekane ananishinda kimasomo. Namshukuru Mungu hawa watuwalinisaidia sana kuinuka kimasomo.

Kuna wanafunzi waliokuwa madarasa ya juu yangu ambao walikuwa na akili sana na walikuwa wakizawadiwa kila mwisho wa mwaka kwa kupewa daftari na kalamu, watu hao ni Musa Mtambalike, Tadeo Sanga (mtoto wa mjomba wangu), Marehemu Emilio Mbilinyi. Nilitamani sana kuwa kama wao nah ii ikanisababishia mimi kusoma kwa juhudi sana.

Kipindi tunasoma tulikuwa hatuna tuition wala muda wa kujisomea tukitoka darasani. Mara nyingi mwalimu anapokuwa darasani ndipo tunakuwa makini katika kusoma au pale mwalimu anapotupa muda wa kujisomea. Tukirudi nyumbani tunaachana na masomo na kufanya kazi za nyumbani kama kuchota maji, kukata kuni msituni, kulima na kazi zingine nyingi. Maisha hayo yalikuwa ya kawaida sana na hakuna mtu aliyekuwa anashangaa juu ya hilo.

Nilipofika darasa la sita nilichanguliwa kuwa mtunza muda au mgonga kengere . Wajibu wangu ulikuwa kugonga kengere ya saa 1 au 12 asubuhi ili wanafunzi waweze kuhesabiwa namba, kugonga kengere za vipindi, kugonga kengere kwaajili ya kuwaruhusu wanafunzi kwenda nyumbani. Wanafunzi walionekana kuchelewa walipewa adhabu kama kupigwa viboko, kulima mashamba, kuleta mzigo wa nyasi na adhabu nyingine nyingi.

Nilichukia sana kazi hii kwani ilikuwa inanilazimu kuamka asubuhi na mapema, na kuwepo shule muda wote kwani sikuweza hata kutoroka.

Kuna marafiki zangu ambao sitawasahau kama vile Nasa, jamaa huyu ni moja ya wanafunzi waliokuwa watoro sana shule, alikuwa anashinda msituni akiwinda. Pia kuna rafiki yangu Paskari Cahaula, huyu alikuwa naye mtoro sana na mgomvi sana, wanafunzi tulikuwa tukimuogopa sana kutokana na ukatili wake.

Kuna michezo Fulani ambayo ilikuwa ikinifurahisha sana nikiwa shule ya msingi. Tulikuwa tukiwakamata wasichana na kuwalaza chini na sisi kuwaangukia juu, na hii ilikuwa ikifanyika wakati wa kwenda nyumbani baada ya masomo kuisha. Tulikuwa tunaweka kioo chini ya miguu ya wadada na kuwachungulia.

Nawakumbuka walimu wangu waliokuwa wakinifundisha nikiwa darasa la kwanza; Mwalimu Mlula (alinifundisha Kiswahili) , Marehemu Mwalimu Mpiluka (alinifundisha Mwandiko na Hesabu).  Kuna walimu wengine walionifundisha kuanzia darasa la pili mpka la saba ambao ni Mwalimu Mkuu Kondo na baadae alihama nakuja Marehemu Mwalimu Mkuu Ndelwa, Marehemu Mwalimu Mveyange ambaye alikuwa mlemavu wa mguu mmoja, Marehemu Mwalimu Namanga, Mke wa Mwalimu Ndelwa (alinifundisha Sayansi), Mwalimu Onesmo (alinifundisha Jiografia), Mwalimu Rashid (alinifundisha hesabu), Mwalimu Mpinda (alinifundisha Michezo) na wengine  

Nakumbuka nikiwa kijijini hapo, nimelima sana, nimewinda sana, na shughuli nyingi unazozijiua za vijijini. Nakumbuka wakati wa jumamosi nilikuwa naongozana na rafiki zangu kama Hadija Chaula, Ombeni Sanga, Rashid Chaula, Mashaka, George Sanga, marehemu Silvatus Mtavangu, na wengine wengi tunaelekea katika mto mmoja ulikuwa unaitwa Mbalue kufua nguo. Kutoka katika makazi mpka kufika katika mtu huo ni mbali kidogo, kwahiyo usafiri wetu ulikuwa ni baiskeli na mbao “Vigereti” au troli za mbao.

Basi tukifika mtoni hapo, sabuni tuliyokuwa tunatumia ni majani yaliyokuwa yanaitwa “majani ya mtavangu”. Majani hayo ukiweka kwenye maji na kufikicha yanatoa povu. Tulipenda sana kuongelea katika mto ule, na bila kuogopa nyoka za majini hata kama kuna siku zingine zilikuwa zikionekana.

Niliyafurahia sana maisha yale, kwani kulikuwa na hali fulani ya upendo kati yetu. Mbali na kufua nguo zetu, pia kulikuwa na shughul zingine nilizokuwa nikifanya na rafiki zangu hasa kipindi cha wikendi. Tulikuwa tunafunga safari kwenda kununua matunda damu katika kijiji cha Ikonongo na umbali mkubwa sana, na hatukuwa tunatumia usafiri wowte zaidi ya kutembea kwa miguu. Matunda hayo tulikuwa tukiyanunua na kuyauza.

Kuna baadhi ya kazi tulizokuwa tukiwa tunasoma na zilitokea kunikera sana. Baadhi ya kazi hizo ni kulima mashamba ya shule, kufanya vibarua vya shule kwa kulima au kupalilia miti au mhindi katika mashamba makubwa kama ya marehemu Mlumbe, Marehem Lusan Sanga (mjomba wangu), mashamba ya chai ya Itona (kuchuma chai) na mashamba ya watu wengine. Tulikuwa tunashinda mashambani kuanzia asubuhi hadi jioni. Kuna siku zingine tunaingia shambani jioni. Kazi hizi nilizichukia sana.

Nikiwa bado darasa la sita, nilichaguliwa kuwa mmoja wa wasaidizi wa Mapadre ambao walikuwa wakitokea Parokia ya Mafinga na kuja kuhubiri kanisani kwetu Mtili “A”. Niliipenda sana ile kazi kwani nilikuwa karibu sana na Wazungu na Wahindi. Kijijini kwetu kuwa karibu na mzungu ulionekana mtu wa maana sana. Namshukuru sana Katekista Kalinga ambaye kwa sasa ni marehemu. Tulikuwa tunasaidiana na motto wa katekista Fredy Kalinga ambaye na yeye ni marehemu. Tulipenda sana na Fredy na baba yake alitokea kunipenda kutokana na tabia yangu nzuri mbele za watu.

Nilipofika darasa la saba nilijiibidiisha sana kimasomo, nilitamani sana kusoma. Kuna vitu vilikuwa ninanikera sana katika elimu yangu. Nikiwa nyumbani sikuweza kusoma usiku kutokana na kukosa taa ya kusomea, nikibahatika nilikuwa natumia kibatali ambacho kilikuwa kikitoa moshi mzito sana, na chumba kinajaa moshi.

Siku moja kaka yangu Amir sanga ambaye ni marehemu aliona ile hali hakupendezewa na kuahidi kuninunulia taa ya chemli, na hii ilinisaidia sana kwani nikawa sipati moshi kabisa. Kijiji nilizidi kuheshimika kwani ni watu wachache wanaotumia taa ya chemli.

Siku ya mtihani wa darasa la saba ulipofika, Mwalimu namanga na Mwalimu Mrs. Ndelwa (mke wa mwalimu mkuu) walikuja ghetoni kwangu usiku na kuniambia siku ya mtihani nisihofu sana na nisipaniki, maana walijua hali yangu na bidii zangu katika masomo. Siku ya mtihani ilipofika nilifanya vizuri na ninamshukuru sana Mungu nilifaulu na kujiunga na shule ya sekondari ya Njombe  mkoani Njombe.

Inaendelea...

MAISHA YA SHULE NIKIWA SHULE YA SEKONDARI NJOMBE.

RULEA SANGA KIPINDI YUKO SHULE YA SEKONDARI NJOMBE (NJOSS) 1995-1998 KIDATO CHA KWANZA HADI CHA NNE

 Rulea wa pili kutoka kushoto nikiwa Mbeya kipindi cha likizo
 Rulea Sanga niliyevaa sandos nikisoma bwenini
 Rulea Sanga kushoto nikiwa na kikundi cha Tambaza. Kutoka kulia ni Allen Mwihava, wa tatu ni Nasoro, Tryphone na Embagise

 Rulea sanga kulia nikiwa na rafiki yangu niliyempenda sana shuleni
 Rulea sanga nikiwa na marafiki zangu, kulia ni Samy ambaye kwa sasa ameokoka, Yusuph
Nikiwa Disko
 Rulea sanga katikati katika mapozi..Mungu anisaidie
 Rulea sanga wa pili kutoka kushoto nikiwa na rafiki zangu Mbeya kipindi cha likizo
 Rulea Sanga wa pili kushoto nikiwa na rafiki zangu wa kidato cha pili
 Rulea Sanga wa tatu kutoka kushoto nikielekea mjini kuzurula wakati wenzangu wako darasani
 Rulea Sanga wa pili kutoka kulia nikionyesha mapozi ya mamtoni, na rafiki zangu wa Tambaza
 Kutoka kushoto ni Fikiri, Simon (niga), Deo ambaye alipata Division One, Rulea Sanga
 Rulea Sanga wa pili kutoka kulia nikiwa na class mate zangu. Kulia ni Samy Black
 Rulea Sanga kulia, nikiwa najisomea na rafiki yangu Fadhili Rwendo ambaye sasa hivi ni Mwanashera (Wakili)
 Rulea sanga wa pili kutoka kushoto, wakati wa gradution yangu kidato cha nne
 Rulea sanga nikiwa katika gari la Marehemu kaka yangu Amir Sanga maeneo ya Mafinga Iringa wakati wa likizo
 Nikipata chakula cha jioni katika Dinning Hall NJOSS
 Rulea Sanga wa tatu kutoka kushoto nikiwa na kundi la Tambaza
 Rulea Sanga, kulia nikiwa na wadogo zangu wa kidato cha pili, wakati mimi nikiwa kidato cha tatu
 Rafiki yangu Tryphone ambaye aliruka na Division One kidato cha nne wa kwanza kulia
Nikiwa katika bustani yangu-NJOSS
 Kikundi kutoka Tambaza
 Rulea sanga wa pili kutoka kushoto nikiwa kidato cha pili na classmate wangu
 Nikiwa kidato cha nne, niliyechuchumaa

ANGALIA PICHA
Rulea Sanga ndani ya Mafinga mkoa wa Iringa maeneo ya Mkombwe

 Rafiki yangu niliyempenda sana wa kitaa, anaitwa Sebastian. Huyu jamaa alikuwa kichwa sana Chuo Kikuu ila watu walimchezea akawa chizi. Ila kiingereza usimguse
 Nikiwa kanisani Mafinga kipindi cha likizo, niliyechuchumaa
 Katikati ni Rulea sanga nikiwa na rafiki zangu, Tryphone (kushoto) na Sanjigwa
 Nikiwa katikati na classmate, kushoto ni Onesmo Mhewa ambaye aligonga Division One kidato cha nne
 Nikipiga Basketball
Rulea Sanga nikivalishwa taji wakati wa garaduation yangu ya kidato cha nne. Kushoto ni Timoth
 Rulea nimkiwa katika pozi ambalo silielewi kiukweli
 Rulea sanga kulia nikiwa bwenini na David Mhonzo


 Rafiki yetu alitutoka shuleni Njombe na kupelekwa kuzikwa kwao Mbeya
 Nikiwa maeneo ya Mafinga sokoni na rafiki yangu kipindi cha likizo
 Nikiwa disko katika ukumbi wa shimoni kwa No Sweat Mafinga kipindi cha likizo
Rulea Sanga aliyevaa kofia akiwa na marafiki zake wakifanya pikiniki mkoani Njombe. Kulia ni classmate David
Rafiki zangu wakiwa bwennini namba 5. Asili yao ni watu wa Mbeya. Sam (Panagamawe) kulia
 Nikiwa Disko Mafinga katika ukumbi wa hospitali ya Mafinga kipindi cha likizo

Kulia ni Rulea Sanga na David Muhonzo
Rulea kulia nikiwa na rafiki yangu (mtalaamu wa mpira wa kikapu). Tupo dukani kwa marehemu kaka yangu Amiri Sanga Mafinga Iringa
 Rulea Sanga nikiwa katika korido karibu na darasa langu. Nyuma yangu ni Justin Sanga
Rulea Sanga katika pozi katika korido la darasani kwangu Njombe (NJOSS)
Kulia ni rafiki yangu niliyempenda sana shule nzima Michael Mtweve
Rulea Sanga kushoto na Justin Sanga mkoani Njombe shuleni NJOSS
Rulea Sanga na David Muhonzo mkoani Njombe (NJOSS)
Rulea Sanga (kulia) na mtoto wa kaka yangu Daniel Sanga

MAISHA YA HIGH LEVEL KATIKA SHULE YA JITEGEMEE MGULANI DAR ES SALAAM
Kulia ni Rulea Sanga na classmate wangu
Rulea Sanga wa pili kutoka kulia nikiwa na Simon, Omary Kaseko ambaye kwa sasa anaishi Marekani
Rulea Sanga kushoto nikiwa na Samy Jabir katika birthday ya rafiki
Rulea Sanga (kushoto) nikilishwa keki na rafiki yangu Japhate katika siku ya kuzaliwa ya rafiki yetu baada ya kumaliza kidato cha sita, kipindi hiki nilikuwa naishi kwa huyu rafiki yangu